Home » » MRADI WA MAJI UJUNI MAKETE WAAGIZWA KUTEKELEZWA MAPENA

MRADI WA MAJI UJUNI MAKETE WAAGIZWA KUTEKELEZWA MAPENA

Written By kitulofm on Thursday, 6 March 2014 | Thursday, March 06, 2014

Serikali wilayani Makete kupitia mhandisi msaidizi wa Idara ya maji imeagiza kampuni ya ZUBERI inayoshughulikia mradi wa utandazaji wa mabomba katika kijiji cha Ujuni kata ya kitulo kukamilisha mradi huo mara moja

Agizo hilo limetolewa Mhandisi msaidizi idara ya maji wilaya ya Makete Bw.Martin Luvanda mapema hii leo katika kijiji cha Ujuni kata ya Kitulo wilayani Makete Mkoani Njombe alipotembelea katika kijiji hicho ili kukagua hatua iliyofikiwa na mkandarasi anayetekeleza  kutoka katika kampuni ya ZUBER Bw.Thomas Maduhu

 Bw.Maduhu ambaye ndiye anayetekeleza mradi huo chini ya usimamizi wa kampuni ZUBERI ameeleza kuwa umalizikaji wa utandazaji wa mabomba hayo kuwa umechelewa kutokana na kucheleweshwa kwa fedha ya kuwalipa vibarua watakaoweza kutandaza na kufukia mabomba hayo
Naye Afisa mtendaji wa kata hiyo Bw.Christopha Fungo ameuomba uongozi wa serikali kutoka halmashauri ya wilaya kuusimamia mradi huo kwa ukaribu zaidi ili mradi huo uweze kukamilika mapema

Mradi huo unaotegemewa kugharimu zaidi ya sh.milioni mia 2 huku ikiwa imeshatumika zaidi ya milioni 70


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm