Mhariri wa gazeti la daraja Letu Robert Zephania (kulia) akimsikiliza mmoja wa maripota akichangia mada katika mafunzo hayo.
Maripota wakimsikiliza kwa umakini Mhariri
wa gazeti la daraja letu Robert Zephania
Edwin Moshi Mmiliki wa mtandao wa EDDY BLOG,akifafanua jambo kwa maripota wa gazeti la Daraja letu.
Picha na Edwin Moshi
Habari na Furahisha Nundu
Zaidi
ya maripota 22 kutoka katika baadhi ya kata zilizopo wilayani Makete wamepata
mafunzo ya siku moja jinsi ya kuandika habari za maeneo wanayoishi kutoka
Gazeti la Daraja lililopo Mkoani Njombe
Akizungumza
katika mafunzo hayo Mhariri wa gazeti la Daraja letu Robert Zefania amesema
kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuongeza ufahamu kwa jamii ya wanamakete na
watanzania kwa ujumla kwani gazeti hilolimekuwa likitoa changamoto
zinazoikabili jamii na wahusika huzifanyia kazi
Akielezea
baadhi ya faida zilizopatikana tokea kuanzishwa kwa gazeti hilo
amesema kuwa gazeti limekuwa likiibua changamoto nyingi lakini wahusika
wamekuwa wakizitendea kazi mara moja ikiwemo wananchi waliokuwa wakilalamikia
mbolea aina ya minjingu mara baada ya gazeti hilo kuandika habari hizo serikali imeruhusu
mwananchi kuchagua mbolea anayohitaji
Katika
mafunzo hayo aliongozana na mwanahabari wa Gazeti hilo Shaban Lupimo ambaye
amewaasa maripota hao kufanya kazi kwa kuzingatia maadili
waliyopewa,kujiamini,kuandika habari zenye ukweli na uhakika ili kutoleta
madhara kwa jamii na msuguano kati yake na chanzo chake cha habari
Maripota
hao waliotoka katika kata ya Bulongwa,Matamba,Tandala,Mang’oto,Ukwama ,Lupila
,Ipepo,Ipelele,Iniho,Isapulano,Luwumbu pamoja na Iwawa wamelishukuru gazeti
hilo kwani limewajengea uwezo mkubwa wa kujua jambo na kutambua haki za
wananchi
0 comments:
Post a Comment