Home » » UNYANYASAJI WA JINSIA IRINGA UNACHANGIWA NA MAZINGIRA HATARISHI

UNYANYASAJI WA JINSIA IRINGA UNACHANGIWA NA MAZINGIRA HATARISHI

Written By kitulofm on Wednesday, 19 March 2014 | Wednesday, March 19, 2014

Na Yonna Mgaya IRINGA

Mazingira hatarishi na matatizo ya kisaikolojia ni miongoni mwa mambo yanayopelekea vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ikiwemo ubakaji.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi amesema baadhi ya watu wamepelekea kufanyiwa vitendo vya unyanyasi wa kijinsia kwa kuweka mazingira hatarishi.

Amesema ili kuepusha vitendo vya ukatili ni vyema jamii ikatambua elimu ya ulinzi na salama kwa kutembea kwa makundi nyakati za usiku kwa lengo la kupambana na vitendo hivyo.

Kamanda Mungi amesema uwepo wa vitendo vya kujitoa maisha ikiwemo kujinyonga mkoani Iringa kumetokana watu kuwa na maisha duni, kukosa matumaini ya kupona na msongo wa mawazo.


Hata hivyo, Kamanda wa jeshi la polisi amesema jeshi lake linaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu elimu ya kujitambua kwa lengo la kupunguza matukio ya uharifu ndani ya jamii.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm