Home » » MKUU WA USALAMA WA TAIFA ATEKWA NYARA LIBYA

MKUU WA USALAMA WA TAIFA ATEKWA NYARA LIBYA

Written By kitulofm on Monday, 18 November 2013 | Monday, November 18, 2013


Naibu  mkuu  wa  usalama  wa  taifa  nchini  Libya  Mustafa Noah  ametekwa  nyara  nje  ya  uwanja  wa  ndege wa kimataifa  mjini  Tripoli. 

Mustafa Noah  hakuwa  na  walinzi wakati  alipokamatwa  na  hakuna  kundi  hadi  sasa lililodai  kuhusika  na  tukio  hilo.

 Viongozi  wa  mji  wa Tripoli  jana  walitoa  wito  wa   kufanyika  maandamano  na migomo  kwa  wenye  maduka, shule na  vyuo  vikuu kuilazimisha  serikali  ya  Libya  kuyaondoa  makundi  ya wanamgambo.

 Makundi  hayo  yanalaumiwa  kwa kuhusika katika  mapigano siku  ya  Ijumaa  na  Jumamosi  ambapo watu  46  wameuwawa.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm