Home » » RC NJOMBE AAGIZA KUKAMATWA WAZAZI WA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI NINGA KWA UTORO WA WATOTO WAO NA KUFELI MITIHANI

RC NJOMBE AAGIZA KUKAMATWA WAZAZI WA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI NINGA KWA UTORO WA WATOTO WAO NA KUFELI MITIHANI

Written By kitulofm on Tuesday, 5 November 2013 | Tuesday, November 05, 2013


 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi Akiwakagua wanafunzi wa Shule ya Msingi Ninga Leo.


Mkuu wa Mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi Ameuagiza Uongozi wa Kata ya Ninga Kufuatilia Wanafunzi Wote Wanaoshindwa Kusoma na Kuandika Pamoja na Watoro Katika Shule ya Msingi Ninga Kufuatia Kuwepo kwa Wanafunzi Wanaokariri Miaka Mingi.

Agizo Hilo Amelitoa Leo Wakati wa Ziara yake ya Siku Tatu Katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Ambapo Pamoja na Mambo Mengine Alifanya Ziara ya Kushtukiza Katika Shule Hiyo na Kubaini Baadhi ya Wanafunzi Kushindwa Kusoma na Kuandika Hali Inayopelekea Kurudia Darasa Miaka Mingi.

Aidha Kaptain Mstaafu Asseri Msangi Amesema Uongozi wa Kata Hiyo ni Lazima Uwakutanishe Wazazi wa Watoto Hao Pamoja na Walimu Ili Kufanya Uchunguzi wa Kina Unaosababisha Kufeli Kwa Wanafunzi Hao na Kutoroka.

Katika Hatua Nyingine Captain Mstaafu Msangi Ameagiza Kila Shule Ihakikishe inaweka Shelfu za Vitabu Kwa Kila Darasa Kwani Serikali Ipo Mbioni Kugawa Vitabu vya Kutosha Kila Shule Ambapo Matunzo Makubwa ya Vitabu Hivyo Yanahitajika.

Mbali na Hayo Lakini Pia Amesema Suala la Uhaba wa Madawati Katika Shule za Msingi na Sekondari Mkoani Njombe Haliwezi Kuvumilika Kutokana na Mkoa Kuzalisha Kwa Wingi Zao la Mbao na Kuliuza Katika Mikoa  Mingine na Nchi Jirani.



Hatua hiyo imekuja baada ya kubaini Wanafunzi Sita Kukaa Kwenye Dawati Moja katika Shule ya Msingi Ninga Katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Leo.
 
Na   Gabriel  Kilamlya Njombe. 
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm