Home » » UFUGAJI WA NYUKI MKOANI NJOMBE WAANZA IKIWA KUNACHANGAMOTO

UFUGAJI WA NYUKI MKOANI NJOMBE WAANZA IKIWA KUNACHANGAMOTO

Written By kitulofm on Wednesday, 26 March 2014 | Wednesday, March 26, 2014

 Baadhi ya Mizinga ya Nyuki katika Kikundi cha Mshikamano Katika Kijiji cha Iyayi Wilayani Wanging'ombe


Na Gabriel Kilamlya Wanging'ombe

Wanachama wa Kikundi cha Ufugaji Nyuki cha Mshikamano Kilichopo Katika Kijiji cha Iyayi Wilayani Wanging'ombe Mkoani Njombe  Kimetajwa Kukabiliwa na Uhaba wa Mtaji wa Kuongeza Mizinga Ya Nyuki Ili Iweze Kufikia Mizinga Mia Tano.

Hadi Sasa Kikundi Hicho Kimefanikiwa Kumiliki Mizinga 225  Ya Nyuki Ambayo Imetolewa na Wafadhili Katika Kuwakwamua Wananchi Kiuchumi.

Akizungumzia Hali ya Kikundi Hicho Mwenyekiti wa Kikundi Bwana S-----Sungura Amesema Kuwa  Kikundi Hicho Tangu Kianze Mwezi April 17 Mwaka 2013 Kimefanikiwa Kupa Fedha Kiasi Cha Zaidi ya Shilingi Milioni Mbili Kutokana na Mavuno Ya Asali.

Akizungumzia Suala la Ufugaji Nyuki Katika Kikundi Hicho Mkuu wa Mkoa wa Njombe Capteni Mstaafu Asseri Msangi Amewataka Wataalamu wa Nyuki Kuhakikisha Wanasaidiana na Wananchi Katika Kuhakikisha Wanafuga Kitaalamu Ili Waweze Kupata Asali Nyingi Zaidi.

Aidha Msangi Amewashauri Wananchi Hao Kuboresha Maeneo Ya Ufugaji wa Nyuki Hao Kutokana na Hali Ya Mvua Zinazoendelea Kunyesha Ili Kuongeza Kiwango cha Uzalishaji wa Asali.
CHANZO:EDDY BLOG
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm