Home » » BUNGE MAALUM LA KATIBA MWENDO MDUNDO LICHA YA UPINZANI KUSUSIA JANA

BUNGE MAALUM LA KATIBA MWENDO MDUNDO LICHA YA UPINZANI KUSUSIA JANA

Written By kitulofm on Thursday 17 April 2014 | Thursday, April 17, 2014



Vikao vya Bunge Maalum la Katiba vimendelea tena leo kwa kujadili sura ya 1 na ya ile ya 6 ya Rasimu ya Katiba licha ya baadhi ya wajumbe kususia kikao hicho jana jioni na kutoka nje ya ukumbi kwa kile walichodai ni kuchoshwa na matusi, dharau na ubaguzi .

Kauli ya kuendelea kwa kikao leo ilitolewa usiku wa jana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Federick Werema  kabla ya kuahirishwa kwa kikao cha jioni cha Bunge hilo, wakati aliposimama kutoa hoja ya kutengua Kanuni za Bunge Maalum la Katiba ili kuongeza muda wa kujadili sura hizo, kutoka 3 hadi siku saba.

Kabla kutengua, Werema alisema mizaha katika Bunge hilo haina tija, hivyo kususia kwa baadhi ya wajumbe hakuzuii kuendelea kwa majadala huo.

“Ninawaomba waliokubali kuendelea na mjadala huu tuwahi kesho,” alisema Jaji Werema.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hassan aliwataka wajumbe hao kuwahi mapema saa 3:00 asubuhi ili kuendelea na kikao.

Kuhusu ombi la mwongozo kutoka kwa mjumbe wa Bunge hilo, Mwigulu Nchemba kuhusu kitendo na hatima ya wajumbe waliosusia kikao na kutoka nje, Makamu Mwenyekiti huyo alisema itajulikana baaada ya Kamati ya Uongozi wa Bunge Maalum la Katiba kukutana. 
NA EDDY BLOG
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm