Home » » WANAWAKE 8,500 HUFARIKI KILA MWAKA KWA SABABU YA UJAUZITO NCHINI TANZANIA

WANAWAKE 8,500 HUFARIKI KILA MWAKA KWA SABABU YA UJAUZITO NCHINI TANZANIA

Written By kitulofm on Thursday 17 April 2014 | Thursday, April 17, 2014

Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Evidence for Action (E4A) Tanzania,Craig John Felar, akitoa mada yake juu ya kampeni ya ‘Muokoe Mama muokoe mtoto mchanga’ (Mama ye) kwenye semina iliyohudhuriwa na baadhi ya viongozi kutoka vilabu vya waandishi  habari mikoa mbalimbali nchini .Semina hiyo ya siku mbili iliyoandaliwa na UTPC,ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Lion hotel jijini Dar.
DSC07908
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vilabu vya waandishi wa habari Tanzania ,wakifuatlia mada zilizokuwa zikitolewa kwenye semina ya uhabarisho juu ya kampeni ya ‘Muokoe Mama na Mtoto Mchanga’ inayosimamiwa na shirika lisilo la kiserikali la Evidence for Action (E4A) Tanzania likishirikiana na Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC).
DSC07921
DSC07925
Bango linalohamasisha ushiriki wa kampeni ya ‘Muokoe Mama na Mtoto Mchanga’(mama ye).(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu,

SHIRIKA Lisilo la kiserikali la Evidence for Action (E4A) Tanzania limesema wanawake wajawazito 8,500 kufariki dunia wakati wa ujauzito au kwa matatizo ya uzazi kila mwaka nchini.

Hayo yamesemwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa (E4A) Tanzania, Craig John Felar wakati akiwahabarisha baadhi ya viongozi wa vilabu vya waandishi wa habari nchini juu ya kampeni ya ‘Muokoe mama na Mtoto Mchanga’

Aidha,amesema watoto wachanga 50,000,hufariki dunia ndani ya mwezi wa kwanza baada ya kuzaliwa.

“Kutokana na takwimu hizo,kwa mwaka Tanzania,inapoteza wakazi wote  wa vijiji 20 kama wakazi wake wanakuwa zaidi ya 1300″,amesema.

Amesema waandishi wa habari nchini wanatakiwa kutumia kalamu zao kikamilifu katika kuielimisha jamii juu ya afya ya mama na motto ili lengo la kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga liweze kufikiwa.

Amesema tasnia ya habari nchini inaweza kutoa mchango mkubwa katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga endapo waandishi wa habari watatambua kwamba wanalo jukumu kubwa na kuzuia vifo hivyo kupitia kalamu zao.

Felar alitaja baadhi ya hatua ambazo waandishi wa habari wanaweza kuzichukua katika kusaidia kupunguza vifo hivyo ni kujenga ufahamu miongoni mwa viongozi na jamii kuhusu hatua zinazoweza kuwaokoa watoto wachanga na akina mama wajawazito.

Alitaja hatua zingine kuwa ni kuwahimiza wanawake kujifungulia kwenye vituo vya huduma za afya na si majumbani na kuhamasisha uwepo wa maandalizi ya kumwezesha mama mjamzitio kujifungulia katika kituo cha huduma za afya, Maandalizi hayo yawe ni kwa ajili ya gharama za usafiri,chakula na usindikizaji.

Amesema kutokana na hali hiyo, upo umuhimu mkubwa kwa waandishi wa habari kushiriki kikamilifu na kuhakikisha kampeni ya ‘muokoe mama na mtoto mchanga’,lengo la kupunguza vifo vya nakundi hayo,liweze kufikiwa mapema iwezekanavyo.

Wakati huo huo,Mkurugenzi wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),Abubakar Karsan amesema kuwa umoja huo umeongeza vilabu vipya vya mkoa wa Geita na Simiyu baada kutimiza ya kuwa wananchama.

Amesema kuanzia sasa vilabu vyote vya waandishi wa habari mikoani ambao ni wanachama wa UTPC,vitapatiwa hati maalum kuonyesha kuwa ni wanachama wa UTPC.
CHANZO:MO-BLOG
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm