Home » » IDADI YA VIFO VYA MAFURIKO DAR YAONGEZEKA

IDADI YA VIFO VYA MAFURIKO DAR YAONGEZEKA

Written By kitulofm on Tuesday 15 April 2014 | Tuesday, April 15, 2014

Idadi ya watu waliofariki jijini Dar es Salaam kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika Ukanda wa Pwani Mashariki imeongezeka kutoka wanane hadi kufikia 13.
Mkuu wa Mkoa huo, Saidi Meck Sadiki, alithibitisha kuongezeka kwa watu waliofariki dunia kutokana na mvua hizo zilizoanza kunyesha Ijumaa ya wiki iliyopita.Hata hivyo, alisema hana taarifa kamili ya idadi ya watu walioripotiwa kuathirika na mvua hizo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, alisema miongoni mwa waliokufa  ni pamoja na mtoto Lainat Ramadhan (2), baada ya kutumbukia kwenye shimo lililojaa maji jirani na nyumbani kwao, juzi saa 5:00 asubuhi katika eneo la Chanika Vikorongo, alipokuwa akimfuata mama yake nje.
CHANZO:NIPASHE
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm