Home » » MFUKO WA JIMBO MAKETE MKOANI NJOMBE WAZIDI KUNEEMESHA WANANCHI

MFUKO WA JIMBO MAKETE MKOANI NJOMBE WAZIDI KUNEEMESHA WANANCHI

Written By kitulofm on Monday 21 April 2014 | Monday, April 21, 2014

Zaidi ya shilingi million 30 za mfuko wa jimbo zimetolewa wilayani makete katika kutekeleza miradi mbalimbali katika sekta ya elimu,maji afya, nishati na barabara.

Akitoa taarifa ya ugawaji wa fedha hizo mwenyekiti wa kamati ya ugawaji wa fedha hizo na mbunge wa jimbo la Makete Dr. Binilith mahenge amesema pesa hizo hutolewa kama chachu ya maendeleo na sio kumaliza matatizo kabisa katika jamii na kuwaomba wananchi kurithika na kidogo kilichotolewa.

Nae katibu kamati hiyo ndugu Cyras kapinga ameyataja maeneo yaliyo pata fedha hizo  kuwa ni kata zote wilayani makete katika sekta za elimu, maji, afya ,nishati na barabara,  na baadhi ya wajumbe wa  kamati hiyo akiwemo diwani viti maalum Tarafa ya Magoma Mh Sarah Shembekeza ameushukuru mfuko huo kwa kuwa chachu ya maendeleo wilayani na kuongeza kuwa watendaji katika maeneo tofauti wasimamie kikamilifu fedha hizo
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm