Home » » WAGANGA WA JADI MAKETE WARINDIMA

WAGANGA WA JADI MAKETE WARINDIMA

Written By kitulofm on Monday 21 April 2014 | Monday, April 21, 2014



Kumeibuka ongezeko la waganga wa jadi wilayani Makete mkoani Njombe ambao wamekuwa wakijitangaza kwa kuweka mabango yao ya kujinadi katika nguzo za umeme licha ya sheria na kanuni kukataza wao kujitangaza kwa njia hiyo

Akizungumza na kitulo fm mapema hii leo afisa afya wilayani makete bwana bonifas sanga amesema kisheria  na kanuni  inakataza kutangaza kujitangaza kwa kuweka mabango.

Amesema mganga yoyote anaefika makete anatakiwa kuonana na mganga mkuu wa wilaya ili haweze kukaguliwa vibali vyake kabla ya kuanza kufanya kazi au kutoa tiba na yeye bwana afya anatakiwa kwenda kukagua sehemu ambazo wanafanyia kazi.

Aidha Bwana sanga amesema wataendelea kuwafatilia waganga wa hao wa tiba asili kwa ukaribu na watatoa taarifa kwa wananchi na kuomba wakazi wa makete kuacha tabia ya kukurupukia waganga hao wasio wafahamu wanakotoka.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm