Home » » AJALI MBAYA YATOKEA USIKU WA KUAMKIA LEO MAKETE

AJALI MBAYA YATOKEA USIKU WA KUAMKIA LEO MAKETE

Written By kitulofm on Wednesday, 18 December 2013 | Wednesday, December 18, 2013


 
Hii ndiyo hali halisi ya ajali iliyokuwa pikikipiki imekuwa katika hali mbaya
 Katika hali ambayo ni ya majonzi ajali ya pikipiki usiku wa kuamkia leo saa 4:22 usiku Kta ya Iwawa Makete mjini eneo maarufu kama Kona watu wawili wamegongana uso kwa uso na pikipiki(BODABODA)
 
Katika ajali hiyo pikipiki yenye namba T 280 BJR na nyingine ni T 878 BUK  ,na majeruhi walili waliojeruhiwa vibaya katika maeneo ya kichwa ambapo majeruhi hao ni madereva wa pikipiki hizo walitambuliwa kwa jina moja moja la Ndondola na Mwangadele walifikishwa katika Hospitali ya Wilaya Makete kwa msaada wa wasamalia wema ili kuokoa maisha yao
 
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio wamesema kuwa ajali hiyo imetokea katika eneo baya lenye kona japo kuwa kama madereva hao wangekuwa makini ajali hiyo isinge tokea 
Hata hivyo hadi kitulo fm imefika eneo la tukio polisi walifika mapema na kuweza kuchukua pikipiki hizo kwa kusaidiana na mashuhuda waliokuwepo na kuzipeleka katika kituo cha polisi wilaya ya Makete
Kwa taarifa iliyotufikia hivi punde isiyo rasmi na  chanzo chetu ya habari ni kwamba mtu mmoja ameumia vibaya katika kichwa chake hivyo amepelekwa katika hospitali ya Rufaa Mkoani Mbeya kwa matibabu zaidi
Kwa habari zaidi endelea kutembelea mtandao huu
Na Furahisha Nundu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm