Home » » BREAKING NEWS: AJALI MBAYA YA PIKIPIKI YATOKEA KONA MAKETE USIKU HUU, MADEREVA WAPO HOI

BREAKING NEWS: AJALI MBAYA YA PIKIPIKI YATOKEA KONA MAKETE USIKU HUU, MADEREVA WAPO HOI

Written By kitulofm on Tuesday, 17 December 2013 | Tuesday, December 17, 2013

Habari zilizotufikia usiku huu ni kwamba kumetokea ajali mbaya za pikipiki maarufu kama bodaboda kugongana wilayani Makete mkoani Njombe

Ajali hiyo imetokea usiku huu majira ya saa 4:22 eneo la Kona Makete ambayo imehusisha pikipiki mbili aina ya SANLG zenye namba za usajili T 280 BJR na nyingine ni T 878 BKU

Madereva wote wawili ambao majina yao hayakufahamika mara moja wamejeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Makete kwa matibabu zaidi

Habari zaidi zitakujia muda wowote kuanzia sasa kutoka kwa mwandishi wetu Furahisha Nundu ambaye yupo eneo la tukio
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm