Home » » WASICHANA 700 WAPATA MIMBA,WAACHA SHULE

WASICHANA 700 WAPATA MIMBA,WAACHA SHULE

Written By kitulofm on Sunday, 15 December 2013 | Sunday, December 15, 2013

Zaidi ya wasichana 700 wenye umri kati ya miaka 10 na 19 ambao walikatisha masomo kwa sababu ya mimba katika shule za msingi na sekondari Wilaya ya Kahama, wamejitokeza kupatiwa elimu ya uzazi wa mpango na ujasiriamali inayotolewa na Shirika la Kiota Women Health Development (Kiwohede) la Dar es Salaam.
 
Idadi hiyo ni kubwa ikilinganishwa na wasichana 350 waliopo kwenye bajeti ya mradi, hali iliyoonyesha tatizo hilo kuwa kubwa wilayani Kahama.
Mkurugenzi wa Kiwohede, Justa Mwaituka alisema idadi hiyo ya wasichana 700 waliokatisha masomo imetoka kata nne za Lunguya, Shilela, Mhongolo na Busoka kati ya kata 55 za Kahama, hali ambayo inaonyesha ni hatari.
SOMA ZAIDI:MWANANCHI
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm