Home » » BARABARA ZA MAKETE VIJIJINI TATIZO

BARABARA ZA MAKETE VIJIJINI TATIZO

Written By kitulofm on Friday, 21 March 2014 | Friday, March 21, 2014





Habari na Elia Kimani,Picha na Furahisha Nundu

Wananchi wa kijiji cha Matenga ktk kata ya Ikuwo wilayani Makete mkoani Njombe wameiomba serikali kuwatengenezea barabara ya kutoka ujuni kwenda Ikuwo kwani kuna tatizo kubwa hasa kwa kipindi cha Masika.

Akizungumza kwa niaba ya wananchin wa kata hiyo Diwani wa kata hiyo Mh.Antony Sanga amesema miundombinu ya barabara ktk eneo hilo imekuwa changamoto kwani inapitika kwa shida hasa kipindi hiki cha masika.

Pia amesema kuwa wakazi na wasafiri walio wengi hulazimika kutumia usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda ambapo kutoka Ikuwo kwenda Maakete mjini ni sh.elfu 30 kitu ambacho kwa wanachi wa Makete ni vigumu.

Pamoja na hilo amesema kuna changamoto ya kutokuwepo kwa huduma ya mawasiliano tokea kuanza kwa huduma za simu wananchi wamekuwa wakipata mawasiliano kwa kusimama juu ya miti na milimani.


Hata hivyo ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa kata ya Ikuwo kwa jitihada za kuendelea na ujenzi wa wodi kwani kwa sasa wapo ktk hatua za mwisho za ukarabati wa jengo hilo.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm