Home » » "ULINZI KWENYE MABANDA YA BIASHARA MAKETE NI MUHIMU"

"ULINZI KWENYE MABANDA YA BIASHARA MAKETE NI MUHIMU"

Written By kitulofm on Friday, 21 March 2014 | Friday, March 21, 2014

Na Furahisha Nundu

Wafanyabiashara wenye vibanda  katika kitongoji  cha Dobwela  Kijiji cha Iwawa Kata ya Iwawa  Wilayani Makete  wamewataka wafanya biashara  kuwa na ulinzi  ili kulinda mali zao.

Wameyasema hayo katika mkutano  uliyofanywa na umoja wa  watu wenye vibanda Dobwela  uliofanywa ili kujadiri  jinsi ya kulinda  mali zao  za biashara katika kitongoji hicho.

Mkutano huo uliyo kuwa chini ya  makamu mwenyekiti wa kitongoji hiho Bw.Henry Mahenge ambapo umoja wa wanakikundi hao wamesema ni vema  kuwepo ulinzi katika eneo hilo ili  kufanya biashara zao  kwa amani na umoja bila kuwa na shaka yoyote.

 "Ili tufanye biashara zetu kwa amani ni lazime tuhakikishe tumeweka ulinzi katika eneo hili la Dombwela mbona wenzetu maeneo mengine kama Mabehewani,Sokoni wameweka walinzi?"Alizungumza mmoja kati ya wanye vibanda eneo hilo

Hivyo wameadhimia kuajiri ulinzi  ili wawasaidie kulinda  kwani watakuwa wanachangia  kila mwezi ili kuwalipa walinzi hao  mali zao ziendelee kuwa katika hali ya usalama.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm